Jinsi ya Kupata Wateja na Downline kwenye Network Marketing Tanzania

Mfumo wa kukusaidia kuwafikia watu sahihi, kupata wateja na kujenga downline kupitia biashara yako ya Network Marketing mtandaoni.

Mfumo wa Kuapa Downline na wa bidhaa kwenye Biashara yako ya Network Marketing

Changamoto kubwa ya network marketer wengi inaanzia hapa

Kama unafanya Network Marketing Tanzania, huenda umewahi kupitia hali hii
  1. Unapost content lakini watu wengi wanaishia kuangalia tu.
  2. Unaongea na watu kuhusu bidhaa zako, lakini wachache wanafanya uamuzi wa kununua.
  3. Unapata watu wanaovutiwa na biashara, mnaanza mazungumzo, halafu mawasiliano hayazai matunda uliyo tarajia.
  4. Unapata mtu mmoja anajiunga na timu yako, lakini baada ya hapo unajikuta wewe ndiye unayemtafutia watu, unayemwelekeza kila kitu, na kumsukuma kwenye kila hatua.
Kesho unaanza tena.
  • Unatafuta mtu mwingine.
  • Unaweka post nyingine.
  • Unafanya presentation nyingine.
  • Unafuatilia mtu mwingine.
Na baada ya muda, unaweza kujikuta unafanya kazi nyingi lakini biashara yako bado inakutegemea wewe.
Tatizo linaweza kuwa si bidhaa yako.
Si kwamba watu wote hawana uwezo wa kununua bidhaa au huduma yako.
Wala si kwamba unahitaji tu, kuongeza idadi ya watu unaowafikia.
Unachokosa ni mfumo unaounganisha kila juhudi unayofanya kwenye biashara yako, ili kuwa safari moja ya biashara, inayo muongoza mteja kwa mpangilio.

Mtu kuvutiwa na bidhaa au biashara yako ni mwanzo wa safari, ila kumgeuza kuwa Mteja au Downline ndilo jukumu lako kuu

Mtu anaweza kuona video yako leo.
  •  Akaipenda
  • Akaingia kwenye profile yako kwenye Instagram au facebook.
  • Akaangalia maudhui yako mengine.
  • Akauliza kuhusu bidhaa.
  • Au akaanza kufikiria kuhusu kujiunga na biashara yako.
Lakini kama hakuna hatua inayofuata, kuvutiwa huko kote kunaweza kuishia hapo.
Hapo ndipo Network Marketer wengi wanapoteza watu ambao tayari walikuwa wameanza kuvutiwa na bidhaa au Biashara.
 
Kwa sababu biashara zao zimejengwa kwenye “Nimpate mtu wa kununua bishaa au nimpate mtu wa kujiunga na timu yangu”
 
Badala ya “Nimpate mtu, nimpe kitu cha thamani (Lead Magnet), nichukue mawasiliano yake, niendelee kujenga uhusiano naye na nimuongoze hatua kwa hatua mpaka afanye uamuzi.”
Huo ni utofauti mkubwa.
 
Kwa sababu kupata umakini (attention) ni hatua ya kwanza tu.
Kinachofuata ndicho kinachoweza kugeuza kuvutiwa uko kuwa mauzo au kuwa watu wanaojiunga kwenye biashara yako (downline).

Kama kila mtu mpya anayevutiwa na biashara anakulazimisha uanze mazungumzo upya, biashara yako bado inaendeshwa na nguvu zako, na siyo mfumo.

Hebu angalia biashara yako kwa mtazamo mwingine.
  • Mtu anaona maudhui yako.
  • Anavutiwa na maudhui yako.
  • Anataka kujua zaidi.
  • Anapata taarifa au kitu chenye thamani (Leads Magnet).
  • Anaingia kwenye mfumo wako.
  • Mnaendelea kuwasiliana.
  • Anaanza kukuamini.
  • Anaamua kununua bidhaa au kujiunga na biashara.
  • Kama akiwa sehemu ya timu yako, anafundishwa mfumo wa kufanya kile kile unachokifanya wewe.
Hapo ndipo biashara inaanza kuwa mfumo.
Kila hatua ina kazi yake.
Maudhui hayabebi kazi yote.
Wala WhatsApp, wala Meta Ads,  
Na wewe mwenyewe haupaswi kubeba kila kitu.
Kila sehemu inapaswa kumsaidia mtu kusogea hatua moja ya kuamua kununua bidhaa au kujiunga na Biashara.

Mtu asiponunua leo, haimaanishi amepotea. Huenda bado hujampa sababu ya kukuamini.

Hili ni jambo ambalo Network Marketer wengi hulipuuza.
Mtu anaweza kuvutiwa na bidhaa yako lakini bado hajawa tayari kununua.
  • Anaweza kuwa anataka kujua zaidi.
  • Anaweza kuwa na maswali ambayo hajakuuliza bado.
  • Anaweza kuwa anahitaji muda wa kujifunza zaidi na kuelewa.
  • Anaweza kuwa bado hajui kama bidhaa au biashara yako inamfaa.
Ukiona kutonunua kwake kama mwisho, utarudi kutafuta mtu mwingine mpya.
Lakini ukiwa na mfumo mzuri, unaendelea kumpa sababu ya kukujua, kujifunza kutoka kwako na kuendelea kuwa karibu na biashara yako.
Safari inaweza kuwa kama hivi
  1. Kuona ntangazo lako
  2. Kuvutiwa na bidhaa au huduma yako
  3. Kujifunza zaidi juu ya bidhaa au huduma
  4. Kuzidi Kuwasiliana na wewe
  5. Kuzidi kukuamini
  6. Mwisho wa siku anafanya uamuzi.
Hapo ndipo Maudhui (Content), kitu cha bure cha kuvutia wateja (Lead Magnet), ukurasa wa kupata wateja (Landing Page), WhatsApp na ufuatiliaji (Follow-up) zinapoungana.

Usipofundisha, utalazimika kuuza. Lakini ukifundisha vizuri, utajenga sababu ya watu kukusikiliza.

Maudhui yako haipaswi kuwa sehemu ya kutangaza bidhaa kila siku.
Kwa sababu mtu anayekufuata anahitaji zaidi ya kujua unachouza.
  • Anahitaji kuelewa tatizo lake.
  • Anahitaji kupata majibu.
  • Anahitaji kujifunza.
  • Anahitaji kuona mtazamo tofauti.
  • Na anahitaji kuona kwamba mtu anayezungumza naye anaelewa anachokifanya.
Hapo ndipo content inapoanza kufanya kazi kubwa zaidi kuliko kupata views.
Inajenga uaminifu kabla ya mazungumzo ya mauzo kuanza.
Badala ya mtu kukuona kama mtu anayesubiri tu amuuzie kitu, anaanza kukuona kama mtu ambaye anaweza kumsaidia.

Maudhui yanateka umakini wa watu, lakini ukiwapatia kitu cha bure chenye thamani (lead magnet) itasaidia usiwapoteze

Unaweza kupata views elfu moja.
Lakini kama huna njia ya kuendelea kuwasiliana na watu waliovutiwa, kesho unaweza kuanza tena kutafuta watu wengine watakao vutiwa na bishara yako.
kitu cha bure cha kuvutia wateja (Lead Magnet) inabadilisha hilo.
Unampa mtu kitu cha thamani kinachohusiana na tatizo lake.
Anakichukua.
Anakuachia mawasiliano.
Sasa mtu ambaye alikuwa amekuona kwa sekunde chache anaweza kuingia kwenye mfumo wako wa mawasiliano.
Landing Page inamsaidia kuelewa anachopata na hatua anayopaswa kuchukua.
WhatsApp inakupa nafasi ya kuendelea kujenga uhusiano.
Follow-up inakusaidia kuendelea na mazungumzo kwa wakati unaofaa.
Kwa hiyo mfumo unaweza kuwa katika hatua hizi.
  1. Maudhui (Content)
  2. Kitu cha bure cha kuvutia watu (Lead Magnet)
  3. Ukurasa wa kupata mawasiliano (Landing Page)
  4. WhatsApp
  5. Kutoa elimu
  6. Ufuatiliaji (Follow-up)
  7. Kufanya Maamuzi
Hii ndiyo tofauti kati ya kupata views na kujenga mfumo unaoweza kuzalisha mauzo au Downline kwenye biashara yako.

Sio kufanya kazi zaidi. Ni kufanya kazi kwa mfumo bora.

Ninaamini kufanya kazi kwa bidii ni muhimu.
Lakini biashara inapokua, huwezi kuendelea kuongeza mzigo wa kazi kila siku bila kuboresha namna unavyofanya kazi.
      • Kuna kazi zinazojirudia.
      • Kuna mawasiliano yanayorudiwa.
      • Kuna ufuatiliaji wa wateja (Follow-Up).
      • Kuna taarifa zinazohitaji kupangwa.
      • Kuna maudhui yanayohitaji kutengenezwa.
Baadhi ya kazi hizi zinaweza kusaidiwa na teknolojia na Automation.
Lengo ni kukusaidia kutumia teknolojia pale inapoweza
      1. Kuokoa muda.
      2. Kupunguza kazi zinazojirudia.
      3. Kuboresha mpangilio wa kazi.
      4. Kusaidia ufuatiliaji wa wateja.
      5. Kurahisisha mchakato wa mauzo.
      6. Na kukupa nafasi ya kuzingatia mambo muhimu zaidi ya biashara.
Teknolojia isiwe mzigo mwingine. Itumike kuwa sehemu ya mfumo wa biashara yako.

WhatsApp si mahali pa kumuuliza mtu “Umeamua au Utanunua lini, au Utajiunga lini ?” Ni mahali pa kumsaidia kufanya maamuzi.

Mtu anayekupa taarifa zake za mawasiliano tayari amekupa nafasi ya kuendelea kuwasiliana naye.
Usiitumie nafasi hiyo kutuma ujumbe wa mauzo kila siku.
Anza kwa kuelewa.
  1. Anafikiria nini?
  2. Anahitaji nini?
  3. Ana changamoto gani?
  4. Ni taarifa gani bado hajapata?
Kisha mpe taarifa inayohusiana na kile anachohitaji.
Hapo follow-up haionekani kama kumfuata mtu ili anunue.
Inaonekana kama kuendelea na mazungumzo ambayo yana thamani kwake.
Na automation inaweza kusaidia kazi zinazojirudia, lakini uhusiano wa mtu na mtu bado unahitaji kwa hiyo usije ukaifanya automation kama Mbadala wa kuhusiana na wateja wako

Usiwekeze pesa kwenye matangazo ya kulipia bila kujibu hili swali, Mtu akiona tangazoi langu na kuvutiwa, je nina mfumo wa kumuongoza kwenye hatua nyingine tokea pale

Matangazo ya kulipia yanaweza kufikisha bishara yako kwa watu wengi zaidi
Lakini tangazo likimleta mtu kwenye mfumo usio na mwelekeo, umeongeza tu idadi ya watu wanaouona mfumo wako usiofanya kazi na usitarajie kupata matokeo chanya
Mtu akibofya tangazo lako
  1. Ataenda wapi?
  2. Ataona nini?
  3. Atapewa nini cha thamani?
  4. Je, taarifa zake za mawasiliano zimechukulia?
  5. Je, aliyevutiwa na bidhaa ua biashara amefatiliwa?
  6. Je, unajuaje kama pesa unayotumia inaleta watu sahihi?
Matangazo ya kulipa ili yawe namatokeo chanya lazima uwe na mfumo wa kuwapokea hao waliyovutiwa na bidhaa au huduma na kuwaongoza kwa hatua nyingine mbele zaidi.  
Ndiyo maana matangazo ya kulipia  yanapaswa kuja baada ya kujua
  • Unamtafuta nani ?
  • Unampa nini ?
  • Unampeleka wapi ?
  • Unawasilianaje naye ?
  • Unapimaje matokeo yako. ?

Timu yako hatakuwa kwa kuwapa motisha ya maneno tu. Wafundishe mfumo na wautumie kuendesha biashara.

Mtu akijiunga na biashara yako, usifikirie kwamba kazi imekwisha.
Kazi ya kujenga timu ndiyo inaanza.
Kama kila mtu kwenye timu yako anakutegemea wewe kila siku wanakuuliza?
  • Kaka, nimpateje downline?
  • Kiongozi nitapataje Mteja?
  • Kiongozi nitumie ujumbe gani ?
  • Nifanye nini sasa ?
  • Nimueleze nini ?
Utajikuta unafanya kazi ya watu wengi kwa wakati mmoja.
Na utachoka hata kabla ya kufikia malengo yako.
Lakini ukiwafundisha mfumo
  • Jinsi ya kuwafikia watu sahii mtandaoni
  • Jinsi ya kuwasiliana nao
  • Jinsi ya kutoa kwao kitu cha thamani
  • Jinsi ya kufanya follow-up
  • Jinsi ya kutumia ujuzi wa kidigital kuendesha biashara
  • Jinsi ya kuwafundisha wengine
Unaanza kujenga timu imara inayoweza kufanya kazi kwa weledi.
Lengo si kuwa na watu wengi wanaokusubiri uwaambie cha kufanya.
Lengo ni kujenga watu wanaojua mfumo na wanaoweza kuutumia.

Jifunze kupima matokeo ya juhudi na uwekezaji unaofanya kwenye biashara yako

Unaweza kusema:
  • Nimeweka posts tano wiki hii.
  • Nimeongea na watu ishirini.
  • Nimefanya follow-up.
 
Lakini swali la biashara ni
Kati ya hayo yoteuliyofanya, nini kimetokea au yamezaa matunda gani ?
  1. Ni wangapi walivutiwa na bidhaa au huduma ?
  2. Ni wangapi waliwasiliana na wewe?
  3. Ni wangapi walitaka kujua zaidi?
  4. Ni wangapi walihudhuria presentation?
  5. Ni wangapi uliwafatilia baada ya kuonyesha nia au kuvutiwa?
  6. Ni wangapi walinunua bidhaa au huduma ?
  7. Ni wangapi walijiunga na Biashara?
  8. Na kwenye timu yako, ni wangapi wanaendelea kujenga timu zao pia?
Ukiweza kupima hatua hizi, basi umeacha kuendesha biashara yako kwa kubahatisha.
Kwa sababu unaweza kutambua ni sehemu gani ambayo unapaswa kuboresha. Ili upate matokeo unayotarajia

Juhudi pekee haitoshi kuendesha biashara yako unahitaji mfumo wa kuiendesha.

Hapa ndipo maarifa na ujuzi mbalimbali unapaswa kuunganishwa ili kufanya kazi kwa pamoja.
  1. Copywriting
Inakusaidia kuwasilisha ujumbe unaomfanya mtu asimame na kusikiliza.
 
  1. Maudhui (Content)
Inakusaidia kujenga uaminifu na kutoa elimu.
 
  1. Website na Landing Pages
Zinakupa sehemu ya kumpeleka mtu baada ya kuona tangazo lako.
  1. Kitu chenye thamani unachotoa bure (Lead Magnet)
Inakusaidia kukusanya mawasiliano ya watu wanaovutiwa wa bidhaa au huduma yako.
 
  1. WhatsApp
Inakusaidia kuendeleza mawasiliano na kujenga uhusiano na watu waliyo vutiwa na bidhaa au huduma yako.
 
  1. Matangazo ya kulipia mtandaoni (Sponsored Meta Ads)
Yanakusaidia kuongeza idadi ya watu unaowafikia mtandaoni.
 
  1. Mfumo wa kujenga timu
Unakusaidia kuhakikisha mtu anapojiunga, na timu yako anajua namna ya kuanza na kujenga timu yake pia.
 
Kila ujuzi unathamani yake.
Lakini nguvu yake kubwa iko kwenye jinsi zinavyounganishwa ili kufanya kazi kwa Pamoja (Jinsi zinavyo unganishwa kujenga mfumo wa kuendesha biashara).
Ndiyo maana mafunzo haya hayakufundishi ujuzi huu kama vipande vilivyotawanyika.
Bali mafunzo haya yanakuongoza kwa njia ya vitendo, hatau kwa hatua jinsi ya kuviunganisha kwa Pamoja ili kujenga mfumo mmoja wa kuendesha biashara yako.

Hiki siyo kitabu cha kujisomea tu. Ni mwanzo wa kuiangalia biashara yako kwa jicho la mfumo.

Ndani ya kitabu hiki cha MFUMO UNAOUZA
utaanza kuelewa mambo ambayo yanaweza kubadilisha namna unavyoendesha Biashara yako ya Network Marketing yako mtandaoni
  • Jinsi ya kuacha kutegemea kuuza kila siku na kuanza kutumia maudhui kujenga uaminifu.
  • Jinsi ya kuwafanya watu wanaovutiwa na bidhaa au huduma yako  wasipotee baada ya kuona mahudhui yako kwa mara ya kwanza.
  • Jinsi ya kutumia Lead Magnet na Landing Page kujenga njia ya kuendelea kuwasiliana watu wanaovutiwa na bidhaa au huduma yako.
  • Jinsi ya kutumia WhatsApp kama sehemu ya safari ya mtu kuelekea kufanya uamuzi.
  • Jinsi ya kutumia matangazo ya kulipia mtandaoni, kuongeza kasi ya mfumo wako.
  • Jinsi ya kujenga timu inayojua mfumo, badala ya timu inayokutegemea kwa kila hatua.
  • Na jinsi ya kutumia takwimu au namba kutambua sehemu inayozuia biashara yako kukua. Na kufanya maamuzi ya biashara yako kwa takwimu na siyo kwa hisia.

Usilipie Tsh 200,000/=. Anza kujifunza kwa kulipia Tsh 19,000/=.

Kama umefika hapa, huenda tayari umeona kwamba tatizo la biashara yako linaweza kuwa kubwa kuliko “nipate watu wengi zaidi.”
Unahitaji kujua jinsi ya kuwafikia watu sahihi, kuwapa sababu ya kukusikiliza, kuendelea kuwasiliana nao na kujenga mfumo ambao unaweza kuusaidia wewe pamoja na timu yako.
Ndiyo maana nimeunganisha mafunzo haya kwenye package moja.
Thamani yake yote kwa ujumla ni TSh 736,000/=
Lakini wewe utalipia Tsh 200,000/= tu na utakuwa umeokoa Tsh 536,000/=
Na huhitaji kusubiri mpaka uwe na TSh 200,000/= mkononi ili kuanza.
Unaweza kuanza kwa kulipia TSh 19,000/=
Na wakati ukiendelea na mafunzo utamalizia kiasi kilichobaki.
  • Na ukiona mafunzo yetu hayakusaidii chochote
  • Hakuna thamani yoyote unayoipata kutokana na mafunzo yetu au
  • Uamuzi uliyofanya wa kulipia umefanya kwa Bahati mbaya
Basi utatwambia tukurudishie pesa yako na sisi ndani ya siku zaba tutakurudishia pesa yako bila usumbufu wowote.

Je, nitahitaji muda gani kukamilisha mafunzo haya ?

Ni wiki mbili tu.
Mafunzo yote yana jumla ya takribani saa 112 za kujifunza.
Ukiweka pembeni saa 8 kila siku kwa ajili ya kujifunza na kufanya mazoezi, unaweza kumaliza mafunzo yote ndani ya:
Saa 8 × siku 14 = saa 112
Hivyo, ndani ya siku 14, sawa na wiki mbili, unaweza kuwa umepitia mafunzo yote na kupata ujuzi unaohitaji.
Na kama huwezi kutumia saa 8 kila siku, hakuna tatizo. Unaweza kwenda kwa kasi yako mwenyewe na kumaliza kulingana na muda ulio nao.
Kwa hiyo, huhitaji kusubiri miezi mingi kuanza kuona mabadiliko. Panga muda wako, anza kujifunza, na fuata hatua moja baada ya nyingine.

Unganisha bidii yako na mfumo kuendesha biashara yako ili kupata matokeo bora zaidi.

Jiulize kwa uaminifu
  1. Ninawafikia watu sahihi?
  2. Maudhui yangu yanawafanya watu wanielewe au ninawambi tu ninachouza?
  3. Watu wanaovutiwa wanakuwa sehemu gani ya mfumo wangu?
  4. Ninapataje mawasiliano ya watu wanaovutiwa na kile ninachokiuuza ua huduma ninayo itoa?
  5. Ninawasilianaje nao baada ya hapo?
  6. Ninawasaidiaje kuelewa na kufanya maamuzi?
  7. Mtu mpya akijiunga kwenye Biashara ninamusaidiaje, kupata ujuzi kama niliyo nao wa kuendesha biashara kwa mfumo.
Kama majibu yako hayako wazi, hapo ndipo pa kuanzia.
 
Pakua kitabu hiki bure MFUMO UNAOUZA.
Usisome kama kitabu kingine cha motisha.
Soma kisha linganisha na jinsi unavyo endesha biashara yako.
  • Angalia ni sehemu gani unafanya vizuri.
  • Angalia ni sehemu gani haipo kwenye mlolongo wa uendeshaji wa biashara yako.
  • Angalia ni wapi watu wanaingia lakini wanapotea.
Kisha anza kujenga mfumo wa biashara yako upya au Kuboresha mfumo uliyo nao kwa sasa.
 
Na kama uko tayari kujifunza hatua kwa hatua jinsi ya kuunganisha
Copywriting, Meta Ads, Website/Landing Pages, WhatsApp.
Ili kujenga mfumo wa kupata downline na wateja mtandaoni
Unaweza kuanza mafunzo haya kwa kulipia TSh 19,000/= tu.
 
Kwa sababu biashara yako haihitaji juhudi pekee
Inahitaji mfumo unaojua cha kufanya kwa kila mtu anayevutiwa na biashara yako.
Picture of Joctan Motoka

Joctan Motoka

Digital Marketing Expert I Creative Graphics Designer
Author I Trainer I Network Marketer
Online Entrepreneur

Ninasaidia watu na biashara kutumia ujuzi na teknolojia kufikia wateja wengi zaidi, kuongeza mauzo na kuendesha biashara kwa mfumo bora zaidi.

Bofya hapa Kunipigie

Karibu Tuzungumze Kuhusu, Biashara

Jifunze jinsi ya kutumia ujuzi wa kidigitali kuendesha Biashara yako ya Network Marketing Bure

Si kwamba Biashara ya Network Marketing haifanyi kazi au ni Ngumu.
Bali ni mfumo au njia unazotumia kuendesha Biashara, ndizo hazikupi matokeao.
Maana zimepitwa na wakati/ hazifanyi kazi.

Some of My Story

Subscribe uzidi kupata Taarifa zetu zaidi kwa kujaza fomu hapa chini

    Scroll to Top